• HABARI MPYA

    Sunday, October 26, 2014

    VAN PERSIE AINUSURU MAN UNITED KUZAMA KWA CHELSEA

    BAO la Robin van Persie dakika ya mwisho limeipokonya tonge mdomoni Chelsea baada ya Manchester United kupata sare ya 1-1 katika Ligi Kuu ya England jioni ya leo.
    United walipata bao hilo la kusawazisha baada tu ya beki Branislav Ivanovic kutolewa nje kwa kadi nyekundu. 
    Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Old Trafford, mkongwe Didier Drogba alitangulia kuifungia Chelsea dakika 53 kabla ya Mholanzi, Van Persie kumuokoa Louis Van Gaal na kipigo.
    Mkombozi; Robin van Persie akishangilia baada ya kuifungia Man United bao la kusawazisha leo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN PERSIE AINUSURU MAN UNITED KUZAMA KWA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top