• HABARI MPYA

    Wednesday, October 29, 2014

    RONALDO AMGARAGAZA 'VIBAYA' MESSI TUZO ZA LA LIGA

    NYOTA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amejiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa tena tuzo ya Ballon d'Or kwa mara ya pili mfululizo, baada ya kumpiku mpinzani wake, Lionel Messi katika tuzo za Ligi ya Hispania.
    Mshambuliaji huyo wa Real Madrid ametwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa La Liga usiku wa Jumatatu baada ya kuwafungia mabao 31 katika ligi mabingwa hao wa Ulaya.
    Hilo linaweza kuwa pigo kwa Messi, ambaye alitwaa kila tuzo miaka mitano iliyotangulia. 
    Cristiano Ronaldo (kushoto), akiwa na mpenzi wake Irina Shayk wakati wa kupokea tuzo hizo

    TUZO ZA LIGA 

    Mchezaji Bora: Cristiano Ronaldo - Real Madrid
    Kocha Bora: Diego Simeone - Atletico Madrid
    Kipa Bora: Keylor Navas - Real Madrid (zamani Levante)
    Beki Bora: Sergio Ramos - Real Madrid
    Kiungo Bora wa ulinzi: Luka Modric - Real Madrid
    Kiungo Bora mshambuliaji: Andres Iniesta - Barcelona
    Mshambuliaji Bora: Cristiano Ronaldo - Real Madrid
    Mchezaji Bora wa Afrika: Yacine Brahimi - Granada
    Mchezaji Bora wa Amerika Kusini: Carlos Bacca - Sevilla
    Mchezaji Bora Chipukizi: Rafinha Alcantara - Barcelona (mkopo Celta 2013-14)
    Bao Bora: Cristiano Ronaldo (vs Valencia) - Real Madrid
    Mchezo wa Kiungwana: Ivan Rakitic - Barcelona (zamani Sevilla)
    Ronaldo's 'mule kick' against Valencia which won best goal
    Ronaldo ametwaa pia tuzo ya bao bora la msimu alilofunga dhidi ya Valencia hapa

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2810838/Cristiano-Ronaldo-clinches-La-Liga-best-player-award-ahead-Ballon-d-Or.html#ixzz3HUDGYv9z 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AMGARAGAZA 'VIBAYA' MESSI TUZO ZA LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top