Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
WINGA Simoni Msuva wiki iliyopita alianguka bafuni na kutonesha kiuno chake kilichomuweka nje ya Uwanja kwa wiki mbili, hali iliyomsababisha aendelee kukosekana katika timu yake, Yanga SC.
Hata hivyo, kulingana na maendeleo yake, kuna uwezekano Msuva akarudi uwanjani wikiendi hii, Yanga SC ikicheza na Mgambo JKT Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Msuva amekuwa mpishi mzuri wa mabao katika klabu ya Yanga SC siku za karibuni, na zaidi inaaminika ndiye anayeweza kumlisha mpira ya kufunga mshambuliaji Mbrazil wa timu hiyo, Genilson Santana Santos ‘Jaja’.
Kukosekana kwake, kumemfanya Jaja afunge bao moja tu katika mechi tatu zilizopita, ambalo alifunga Yanga SC ikishinda 3-0 dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
Aidha, mshambuliaji Hussein Javu naye anasumbuliwa na maumivu ya goti- na anatarajiwa kwenda kufanyiwa vipimo wiki hii katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili.
Yanga SC inatarajiwa kurejea Dar es Salaam leo ikitokea Bukoba, ambako Jumamosi ilifungwa 1-0 katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na wenyeji Kagera Sugar.
WINGA Simoni Msuva wiki iliyopita alianguka bafuni na kutonesha kiuno chake kilichomuweka nje ya Uwanja kwa wiki mbili, hali iliyomsababisha aendelee kukosekana katika timu yake, Yanga SC.
Hata hivyo, kulingana na maendeleo yake, kuna uwezekano Msuva akarudi uwanjani wikiendi hii, Yanga SC ikicheza na Mgambo JKT Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Msuva amekuwa mpishi mzuri wa mabao katika klabu ya Yanga SC siku za karibuni, na zaidi inaaminika ndiye anayeweza kumlisha mpira ya kufunga mshambuliaji Mbrazil wa timu hiyo, Genilson Santana Santos ‘Jaja’.
![]() |
| Msuva anaweza kurudi uwanjani Jumamosi |
Kukosekana kwake, kumemfanya Jaja afunge bao moja tu katika mechi tatu zilizopita, ambalo alifunga Yanga SC ikishinda 3-0 dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
Aidha, mshambuliaji Hussein Javu naye anasumbuliwa na maumivu ya goti- na anatarajiwa kwenda kufanyiwa vipimo wiki hii katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili.
Yanga SC inatarajiwa kurejea Dar es Salaam leo ikitokea Bukoba, ambako Jumamosi ilifungwa 1-0 katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na wenyeji Kagera Sugar.



.png)
0 comments:
Post a Comment