• HABARI MPYA

    Saturday, April 21, 2012

    VAN PERSIE ABAMBWA KAMBI YA BARCELONA, AJITETEA


    Van Persie

    NAHODHA wa Arsenal, Robin van Persie ametetea uamuzi wake kutembelea hoteli waliyofikia timu ya Barcelona Jumatano, akiwahakikishia mashabiki wa Gunners kwamba alikwenda kumtembelea mchezaji mwenzake wa Uholanzi, Ibrahim Afellay.
    Tetesi zilivuja kwenye vyombo vya habari kwamba mpachika mabao huyo mwenye umri wa miaka 27 anataka kuhamia Camp Nou.
    Mholanzi huyo alipigwa picha katika kambi ya Barcelona, lakini amesema hakwenda huko kwa nia mbaya.
    Van Persie alisema katika taarifa iliyoifikia bongostaz.blogspot.com kwamba: “Ufafanuzi ni rahisi sana kwa kweli. Rafiki yangu mzuri sana Ibrahim Afellay anachezea Barcelona."
    “Baada ya msimu mbaya kwake akiwa majeruhi kwa muda mrefu, hatimaye alirejea kwenye timu – na alipokuwa nje nilikuwa nawasiliana naye sana tu, lakini sikumuona. Hii ilikuwa nafasi yangu kwenda kumtembelea rafiki yangu wa karibu, kumuonyesha sapoti na kushikamana.
    “Kwa bahati mbaya hii ikabidi iwe hotelini, kwa sababu hakupewa ruhusa kuondoka. Nilikuwa nimevaa traksuti yangu ya Arsenal na tulikaa chini mapokezi kuzungumza na kupata chakula – yeyote angeweza kutuona na hakukuwa na kificho. Nashindwa kupata picha kila mmoja analihusisha hili na kuhama!”
    Van Persie pia aliwaweka wazi  mashabiki kwamba fikra zake juu ya mustakabali wake hazijabadilika katika wiki za karibuni na atatoa msimamo wake mwishoni mwa msimu.
    “Kuetembelea hotelini lilikuwa suala moja la kijamaa na halikuwa na chochote juu ya mustakabali wangu wa kazi,” alisema Nahodha hyuyo.
    “Nina maisha ya kijamaa pembeni ya soka, pia hata kama mke wangu akiniambia hivyo, wakati fulani haionekani kama hivyo! Hakuna kilichobadilika akilini, kwamba nia yangu ni kujadili mustakabali wangu mwishoni mwa msimu,”alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN PERSIE ABAMBWA KAMBI YA BARCELONA, AJITETEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top