• HABARI MPYA

    Saturday, April 21, 2012

    NGORONGORO WAICHAPA SUDAN TAIFA, MGUU MOJA MBELE AFRIKA


    Wachezaji wa Ngorongoro wakishangilia
    TIMU ya taifa ya soka ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes imejiwekea mazingira mazuri ya kusonga mbele katika kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika, baada ya kuibwaga kwa mabao 3-1 Sudan jioni hii, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Shukrani kwao, Thomas Ulimwengu, Ramadhani Singano ‘Messi’ na Simon Msuya walioifungia mabao hayo Ngorongoro inayofundishwa na kocha Mdenmark, Kim Poulsen.
    Kwa matokeo hayo sasa, Ngorongoro inahitaji hata sare au kufungwa si zaidi ya 1-0 kwenye mchezo wa marudiano na Sudan, ambayo jioni hii bao lake la kufutia machozi lilifungwa na Sharafeldin Shaiboub, ili kusonga mbele.
    Ngorongoro wana kazi ngumu bado, kwani bao la ugenini walilopata leo- ina maana wakishinda 2-0 kwenye mchezo wa marudiano kwao, watasonga mbele.
    Pouslen aliiambia bongostaz.blogspot.com kwamba amefurahishwa na matokeo na anawapongeza vijana wake, lakini akakiri ana kazi ngumu bado mbele.
    Poulsen alisema wameiona Sudan inavyocheza na watafanyia kazi mapungufu yao ili kuhakikisha wanaitoa timu hiyo na kusonga mbele.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NGORONGORO WAICHAPA SUDAN TAIFA, MGUU MOJA MBELE AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top