• HABARI MPYA

    Saturday, April 21, 2012

    KANUMBA SASA AWAJAZA WAJANJA FWEZA


    MAREHEMU KANUMBA
    BAADA ya kifo cha nyota wa filamu za Swahiliwood, Steven Kanumba, biashara nyingi zimeibuka zikitumia picha na jina la Kanumba huku familia yake ikishuhudia biashara hizo zikifanyika bila kufaidika na chochote.
    Biashara zilizotawala awali ilikuwa ni fulana, kofia, vitabu, leso na picha zake. Kutokana na hali hiyo, familia yake kupitia Shirikisho la Wasanii (TAFF) ilitangaza biashara hizo kusitishwa mara moja na wale watakaohitaji kutengeneza bidhaa yoyote inayomhusu Kanumba kuwasiliana familia yake kwanza.
    Pamoja na agizo hilo watengenezaji wa vitabu wamekaidi.
    Wiki hii TAFF kutumia kikosi maalum kinachofanya msako na kukamata kazi bandia, imeanza zoezi la kukamata kazi hizo pamoja na vitabu hivyo baada ya kupewa agizo na mama mzazi wa marehemu, Florence Mtegoze, kuwa hawaruhusu chochote kufanyika bila idhini ya familia.
    Kikosi kazi kilifanikiwa kuwakata baadhi ya wauzaji wa vitabu katika maeneo ya Buguruni jijini Dar es Salaam na kufikishwa kituo cha polisi.
    Shirikisho limeanza kazi kulinda haki za wasanii wake kama unavyoona tayari tumefungua kesi kuhusu kazi za marehemu Kanumba zilizochapishwa bila idhini ya familia yake, alisema Rais wa shirikisho hilo, Simon Mwakifwamba.
    Lakini hatuishii hapo tu kwani tayari tuna mkakati wa kuanza pia kukamata kazi bandia za filamu hasa kwa wale ambao watakuwa wakitoa ushirikiano kwa shirikisho ikiwa ni taarifa na kuonyesha hujuma hizo kutoka upande wowote, filamu, vitabu.

    GAZETI LA MWANASPOTI
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KANUMBA SASA AWAJAZA WAJANJA FWEZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top