• HABARI MPYA

    Wednesday, June 16, 2021

    WAZEE WA ‘MIKEKA’ HIZO NDIZO MBINU NA MAARIFA AMBAYO YATAKUWEZESHA KUFANIKIWA KILA UNAPOBETI POPOTE

    KUMEKUWA na wimbi kubwa la ongezeko la wadau katika Ubashiri nchini, lakini hali zao za kutamani kubashiri zimekuwa zikikwamishwa na sito fahamu ya ulewa afifu juu ya michezo hii ya ubashiri, na wengine wamekuwa wakibashiri kwa sababu wamemuona mtu flani anabashiri na anashinda, mbashiri anatakiwa kutambua kuwa kubashiri kunahitaji uvumilivu kwa kuwa sio wewe tu unaohitaji kushinda, wapo wengi nyuma yako nao wanahitaji kushinda kwaiyo mbinu pekee ndio zitakazo mfanya mbashiri kupata bashiri yako.
    Maarifa pekee na mbinu bora ndio jawabu la mchezaji kushinda bashiri zake kinyume na hapo ni kupoteza bashiri yako, Ila watu wengi wamekuwa wakishindwa kupata matokeo pindi wanapo bashiri, kwa kuwa wanashindwa kujua mbinu, wanakosa mikakati sahii watakayo itumia ili iwape matokeo yaliyo sahihi. Kuna mbinu nyingi zinaweza kumfanya mtu ashinde bashiri yake na anatakiwa kupata matokeo kwenye michezo ya kubashiri sio kazi rahisi.


    Ili ushinde na ufanye ubashiri wa uhakika kitu cha kwanza unachohitaji ni kuelewa kanuni za alama za kubashiri Watu wengi wamekuwa wakijiingiza kwenye michezo ya bashiri pasipo kufahamu, namna gani sahihi ya kubashiri. Hali iliyopelekea makampuni mengi ya ubashiri nchini kuandaa tovuti ili kutoa maelekezo na namna gani unaweza kubashili nakuibuka mshindi.
    Awajaishia hapo tu, ili kuhakikisha michezo hii ya kubashiri inakuwa na wadau wengi, kumekuwepo na mafunzo kupitia vyanzo mbalimbali, ikiwepo kuandaa tovuti zinazoelezea na kuonyesha njia sahihi ya kubeti kwa wateja wao.
    Pindi unapojaribu kujua upi ni upande wenye nguvu zaidi, unaangalia vitu viwili. Kwanza angalia alama ambazo zina utofauti mkubwa kati ya alama za kubashiri kati ya timu pendwa na timu dhaifu.
    Pili angalia alama kubwa za kubashiri kwenye matokeo ya sare maana hili humaanisha sare inauwezekano mdogo mno kutokea. Kuna machaguo mengi ya kuchagua na ukajihakikishia ushindi, lakini yote yanahitaji ufahamu wakutosha juu soka, kufahamu wachezaji kwa ubora wa timu na mchezaji mmoja mmoja, ligi unayopendelea kuitumia kipindi utakapokuwa unabashiri.
    Kufahamu mfumo utakao utumia ambao unaona unakupendeza na ni rahisi kwako kubashiri, kuchagua idadi ya timu uliyoifatilia na kuitambua ubora wake dhidi ya mpinzani wake, hakikisha unafahamu vizuri mwenendo wa ligi ambayo timu hiyo, unayoipendekeza unaijua vizuri. Chaguo lako hakikisha linazingatia sana alama zilizotolewa dhidi ya timu husika. Wakati wa kubashiri ni muhimu kuelewa kuwa ipi ni timu pendwa kushinda mechi au mchezo.
    Kwenye kubashiri timu zinazofikiliwa ni timu zinazofanya vizuri, ni timu ambazo zinauwezekano mkubwa wa kushinda mchezo. Baadhi ya mchezo timu zinaweza kuwa na uwiano sawa wa ubora, wakati timu moja inaweza kuwa pendwa na nyingine dhaifu hali hiyo humaanisha ushindi unaweza kwenda upande wowote. Wakati wa kubashiri timu uliyo ichagua unatakiwa kuhakikisha ina uwezekano mkubwa wa kushinda kuliko timu nyingine.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAZEE WA ‘MIKEKA’ HIZO NDIZO MBINU NA MAARIFA AMBAYO YATAKUWEZESHA KUFANIKIWA KILA UNAPOBETI POPOTE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top