• HABARI MPYA

    Friday, June 11, 2021

    HAWA MNIGA AWA MWANAMKE WA KWANZA KUCHUKUA FOMU KUWANIA URAIS WA TFF KATIKA UCHAGUZI WA AGOSTI 7 TANGA


    MWANAMAMA Hawa Mniga amekuwa mwanamke wa kwanza kuchukua fomu kuwania Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika uchaguzi utakaofanyika Agosti 7, mwaka huu Jijini Tanga.
    Amina ni kati ya wadau wapya watatu waliochukua fomu leo zinazotolewa kwa gharama ya Sh. 500,000 - wengine ni mmilili wa klabu ya African Lyon, Rahim Kangenzi na mwanahabari nguli, Ally Saleh.
    Watatu hao wanafanya idadi ya jumla ya wagombea 10 wa nafasi ya Urais, wengine Rais wa sasa, Wallace Karia, Ally Mayay, Deogratius Mutungi, Oscar Oscar, Evans Mgeusa, Zahor Mohamed na Mbunge wa Kinondoni (CCM), Tarimba Abbas.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAWA MNIGA AWA MWANAMKE WA KWANZA KUCHUKUA FOMU KUWANIA URAIS WA TFF KATIKA UCHAGUZI WA AGOSTI 7 TANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top