MATUMAINI ya Manchester City kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya England yamezidi kufifia baada ya usiku huu kufungwa bao 1-0 na Burnely Uwanja wa Turf Moor.
Kipigo hicho kinaifanya City ibaki na pointi zake 58 baada ya kucheza mechi 29, wakiizidi kwa pointi moja Arsenal iliyocheza mechi 29 pia.
Chelsea wanaendelea kujinafasi kileleni kwa pointi zao 63 baada ya kucheza mechi 27, wakati Manchester United ni ya nne kwa pointi zake 53 za mechi 28.
Bao pekee lililoizamisha City leo lilifungwa na
George Boyd dakika ya 61 na sasa kocha Manuel Pellegrini anazidi kukiweka ‘rehani’ kibarua chake Etihad.
Kikosi cha Burnley kilikuwa; Heaton, Trippier, Duff, Shackell, Mee, Boyd, Arfield, Jones, Barnes, Vokes/Ward dk87 na Ings/Reid dk90.
Man City; Hart, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Jesus Navas, Toure/Lampard dk81, Fernandinho, Silva/Jovetic dk74, Dzeko/Bony dk63 na Aguero.

Wachezaji wa Manchester City wakiwa taabani baada ya kipigo cha Burnley
PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2994997/Burnley-1-0-Manchester-City-George-Boyd-screamer-sinks-lacklustre-Blues-hands-title-advantage-Chelsea.html#ixzz3UOYFmwTc


.png)
0 comments:
Post a Comment