• HABARI MPYA

    Sunday, April 22, 2012

    WAZIRI ZANZIBAR AMFICHUA MCHAWI WA SOKA TANZANIA


    Dk Mwinyihajji Makame akizungumza na BIN ZUBEIRY

    WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Dk Mwinyihajji Makame amesema kwamba Tanzania ina vipaji sana vya soka, lakini kwa sasa kinachokosekana ni uongozi bora na ndiyo maana mchezo unashuka.
    Akizungumza na bongostaz.blogspot.com jana katika hoteli ya Zanzibar Beach Resort visiwani Zanzibar, Dk Makame amesema kwamba vipaji vipo, lakini lazima jitihada za kuwekekeza kwenye soka ya Vijana ziwe za dhati.
    Alisema anapongeza sera za sasa za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwamba kila klabu lazima iwe na timu ya vijana ndipo, iruhusiwe kucheza Ligi Kuu, lakini ameomba mpango huo utiliwe mkazo.
    Hata hivyo, Dk Makame amesikitikshwa na desturi ya TFF kuonekana kujali zaidi Simba na Yanga au Dar es Salaam pekee na kusahau mikoa ikiwemo Zanzibar, hali ambayo imechangia kushuka kwa soka ya mikoani na kuathiri maendeleo ya soka ya nchi hii kwa ujumla.
    “Nchi hii ina vipaji sana, tangu zamani, mimi nakumbuka miaka ya 1970 ilikuja hii timu ya West Brom Albion (ya England) ikacheza mechi mbili za kirafiki, ilicheza na timu ya kombaini ya Dar es Salaam, ikacheza na taifa kombaini, ambayo haikuhusisha wachezaji wa Dar es Salaam.
    Ulichezwa mpira mkubwa sana na timu zote zilitoka sare na WBA,” alisema.
    Dk Makame amesema ukirejea Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1980 nchini N igeria ambazo ni fainali pekee za michuano hiyo kwa Tanzania kushiriki, wachezaji wa mikoani wengi walikuwamo kikosini.
    “Kulikuwa kuna wachezaji wa Tanga, Morogoro, Tabora na Zanzibar na kadhalika, haikuwa wachezaji wa Dar es Salaam pekee kama ilivyo sasa.
    Thuwein Ally aliisaidia sana timu na ndiye aliyefunga mabao yetu yote kule, huyu chimbuko lake na hapa (Zanzibar). Sasa lazima TFF iweke mikakati ya kuisaidia mikoa kuzalisha vipaji na kuviendeleza na kuacha kuanglia Dar es Salaam pekee,”alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAZIRI ZANZIBAR AMFICHUA MCHAWI WA SOKA TANZANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top