Manchester United imewafikia kwa pointi mabingwa watetezi, Liverpool baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Aston Villa kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Old Trafford.
Mabao ya Manchester United yamefungwa na Anthony Martial dakika ya 40 na Bruno Fernandes kwa penalti dakika ya 61 wakati la Aston Villa lilifungwa na Bertrand Traore dakika ya 58
Manchester United inafikisha pointi 33 sawa na Liverpool, baada ya timu zote kucheza mechi 16, ingawa mabingwa watetezi wanabaki juu kwa wastani wao mzuri wa mabao PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment