• HABARI MPYA

    Monday, January 11, 2021

    SIMBA SC WAICHAPA NAMUNGO FC 2-1 AMAAN NA KUWAFUATA YANGA FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI

    MABINGWA wa Tanzania Bara, Simba SC wamefanikiwa kwenda fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Namungo FC Uwanja wa Amaan, Zanzibar usiku wa leo.
    Mabao ya Simba SC leo yamefungwa na washambuliaji wake Mnyarwanda, Meddie Kagere dakika ya saba na Miraj Athumani ‘Madenge’ dakika ya 41, wakati la namungo FC limefungwa na Mghana, Steven Sey dakika ya 88.
    Sasa Simba SC watakutana na mahasimu wao wa jadi, Yanga SC Jumatano usiku katika fainali hapo hapo Uwanja wa Amaan.
    Hii inakuwa mara ya nane kwa Simba SC kuingia fainali ya michuano hiyo tangu ianzishwe mwaka 2007 wakiwa wametwaa Kombe hilo mara tatu, 2008, 2011 na 2015 huku 2012, 2014, 2017, 2019 na 2020 wakitoka patupu.
    Kukutana na Yanga SC katika Fainali hii itakuwa mara ya pili baada ya mwaka 2011 Simba waliposhinda 2-0, mabao ya Shijja Mkina na Mussa Mgosi hapo hapo Uwanja wa Amaan.


    ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI
    Mwaka            Bingwa Mshindi wa Pili
    2007 Yanga SC Mtibwa Sugar 
    2008 Simba SC Mtibwa Sugar
    2009 Miembeni        KMKM
    2010 Mtibwa Sugar         Ocean View
    2011 Simba SC  Yanga SC
    2012 Azam FC          Simba SC
    2013 Azam FC    Tusker FC
    2014 KCCA        Simba SC
    2015 Simba SC Mtibwa Sugar
    2016 URA Mtibwa Sugar
    2017 Azam FC Simba SC
    2018 Azam FC URA FC
    2019 Azam FC Simba SC 2-1 
    2020 Mtibwa Sugar         Simba SC 1-0
    2021 ??? ???
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC WAICHAPA NAMUNGO FC 2-1 AMAAN NA KUWAFUATA YANGA FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top