• HABARI MPYA

    Sunday, March 15, 2015

    MAN UNITED ‘MDOGO MDOGO’, SASA WANUKIA ULAYA, WAIBUTUA SPURS 3-0

    MANCHESTER United imeendelea vyema na mawindo yake ya angalau kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa mwakani, baada ya usiku huu kuifunga Tottenham Hostspur mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford.
    Marouane Fellaini aliifungia United bao la kwanza kwa pasi ya Michael Carrick dakika ya tisa. Carrick mwenyewe akafunga la pili dakika ya 19, kabla ya Wayne Rooney kufunga la tatu dakika ya 34.
    Nahodha huyo wa Mashetani Wekundu akakunja ngumi kama anapigana kushangilia bao lake, kuyapoga vijembe magazeti. Kikosi cha Louis van Gaal sasa kimejiimarisha nafasi ya nne, kikiizidi kwa pointi tano Liverpool. 
    Kikosi cha Manchester United; De Gea, Valencia, Jones, Smalling, Blind, Carrick/Rafael dk87, Herrera, Mata/Pereira dk79, Fellaini/Falcao dk83, Young na Rooney.
    Tottenham; Lloris, Walker, Dier, Vertonghen, Rose, Bentaleb, Mason/Lamela dk64, Chadli/Adebayor dk79, Eriksen, Townsend/Dembele dk31 na Kane.

    Wayne Rooney akipiga ngumi baada ya kuifungia Manchester United katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Tottenham leo 

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2995989/Manchester-United-3-0-Tottenham-Marouane-Fellaini-Michael-Carrick-Wayne-Rooney-s-half-strikes-sink-Spurs.html#ixzz3UU1SVSbh 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED ‘MDOGO MDOGO’, SASA WANUKIA ULAYA, WAIBUTUA SPURS 3-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top