• HABARI MPYA

    Sunday, March 15, 2015

    CHELSEA YALAZIMISHWA SARE NA SOUTHAMPTON, 1-1

    CHELSEA imeshindwa kutumia fursa ya kupaa kileleni mwa Ligi Kuu England kwa point inane zaidi, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 Southampton jioni ya leo Uwanja wa Stamford Bridge, London.
    Diego Costa alianza kuifungia The Blues akimalizia krosi ya Branislav Ivanovic dakika ya 11, kabla ya Dusan Tadic kusawazisha kwa penalti dakika ya 19, kufuatia Sadio Mane kuangushwa na Nemanja Matic.
    Ivanovic alilalamika angestahili kupewa penalti kipindi cha kwanza baada ya kuangushwa na Tadic kwenye boksi. Blues sasa inaidizi kwa pointi Manchester City na ina mechi moja mkononi. 
    Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Matic/Ramires, Fabregas, Willian/Cuiadrado, Oscar/Ramires, Hazard na Costa. 
    Southampton; Forster, Clyne, Fonte, Alderweireld, Bertrand, Wanyama, Schneiderlin, S. Davis/Ward-Prowse, Tadic/Djuricic, Mane na Long/Pelle.
    Costa, who was heavily criticised for his midweek performance against PSG, got back in the business of scoring goals



    Mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa akiruka juu kuifungia timu yake katika sare ya 1-1 na Southampton

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2995830/Chelsea-1-1-Southampton-Dusan-Tadic-levels-Diego-Costa-opener.html#ixzz3UTZOg564 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YALAZIMISHWA SARE NA SOUTHAMPTON, 1-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top