• HABARI MPYA

    Monday, April 09, 2012

    BARCA NA VIBONDE KESHO, REAL NA WAPINZANI KESHOKUTWA

    Ronaldo ataibeba Real Jumatano?
    Messi ataendeleza maajabu yake kesho?
    WAKATI ikizidi kukaribiwa na Barcelona kileleni, vinara wa Ligi Kuu ya Hispania, Real Madrid Jumatano wanakabiliwa na mechi ngumu ya wapinzani wa jiji la Madird, dhidi ya Atletico Madrid inayopigana kuvunja rekodi ya kucheza mechi 22 na wapinzani wao hao bila kushinda.
    Sare tatu katika mechi tano zilizopita, limeipunguzia Madrid kiwango cha pointi za kuongoza La Liga kutoka 10 hadi nne, na Barcelona itakuwa mchezo mwepesi tu kesho dhidi ya Getafe nyumbani.
    Madrid watasafiri hadi Uwanja wa Vicente Calderon katika mchezo muhimu zaidi kushinda kuliko hata dhidi ya Barcelona katika wiki zisizozidi mbili.
    “Pengo na Barcelona limepungua, lakini sasa tunatakiwa kuendelea kusonga mbele,” alisema Nahodha wa Madrid, Iker Casillas.
    “Mechi na wapinzani wetu itakuwa maalum. Baada ya muda mrefu wa kutotufunga, kwao utakuwa mchezo muhimu sana kwao.”
    Atletico haijafunga Madrid tangu mwaka 1999 na wanataka kurudi kile kilichofanywa na Valencia Jumapili kutoka sare ya 0-0 na Real.
    Kikosi cha Jose Mourinho, Madrid hadi sasa kimefunga mabao mengi msimu huu, 100 — 74 kati ya hayo yanatokana na Cristiano Ronaldo, Gonzalo Higuain na Karim Benzema—na wanaelekea kuvunja rekodi ya daima ya mabao 107.
    Messi amekwishafanya makubwa na kuvunja rekodi kibao na kesho anatarajiwa kuwa mwiba kwa Getafe.
    Jumamosi Messi alifunga mabao mawili na kuweka rekodi nyingine, kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao 60 katika michuano mikubwa Ulaya, tangu Mjerumani Gerd Mueller afunge 67 alipokuwa Bayern Munich msimu wa 1972-73.
    Muargentina huyo anaongoza kwa mabao La Liga, 38, moja tu zaidi ya Ronaldo, Mreno wa Real. Wote wanawania kuvunja rekodi ya mabao mengi katika La Liga dhidi ya rekodi ya Ligi ya Ureno ya mabao 40 msimu uliopita.
    Mechi nyingine kesho, Osasuna inayoshika nafasi ya sita itakuwa mwenyeji wa Espanyol, wakati Real Betis itakuwa mgeni wa Real Sociedad.
    Valencia wanaoshika nafasi ya tatu watajaribu kuendeleza maajabu yao Jumatano watakapocheza na Rayo Vallecano, ikitoka kupigwa 6-0 na Osasuna mwishoni mwa wiki.
    Levante itasaka pointi mbele ya Sporting Gijon.
    Mechi nyingine Jumatano, Athletic Bilbao itaifuata Granada na Alhamisi Villarreal watamenyana na Malaga; Racing Santander na Mallorca; na Sevilla dhidi ya Zaragoza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCA NA VIBONDE KESHO, REAL NA WAPINZANI KESHOKUTWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top