KLABU ya Newcastle imejiongezea
matumaini ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao, kufuatia ushindi wa tano
mfululizo leo wakati Tottenham ikianza kupoteza matumaini baada ya kufungwa
nyumbani.
Mshambuliaji wa Newcastle,
Papiss Cisse amefunga bao la 10 ndani ya mechi tisa tangu ajiunge na klabu hiyo
Januari mwaka huu, na kusababisha ushindi wa 2-0 kwa Newcastle dhidi ya Bolton,
baada ya Hatem Ben Arfa kufunga la kwanza.
Ushindi huo unawainua The
Magpies hadi nafasi ya tano, nyuma ya Tottenham kwa tofauti ya mabao tu, baada
ya klabu hiyo ya London kuchapwa 2-1 na Norwich.
Anthony Pilkington na Elliott
Bennett waliifungia Norwich, ambayo inaangukia nafasi ya tisa sasa.
Chelsea inaweza kupanda juu ya Tottenham
na Newcastle kama itashinda mechi yake na Fulham inayoendelea hivi sasa.



.png)
0 comments:
Post a Comment