NYOTA Mmisri, Mohamed Salah jana amefunga mabao mawili 57 na 68, Liverpool ikiibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya wenyeji, West Ham United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa London.
Bao lingine la Liverpool lilifungwa na Georginio 'Gini' Wijnaldum dakika ya 84, wakati la Craig Dawson dakika ya 87 na sasa kikosi cha Jugenr Klop kinapanda nafasi ya tatu kikifikisha pointi 40, wakiwa wanazidiwa pointi moja na Manchester United baada ya wote kucheza mechi 21 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment