• HABARI MPYA

    Tuesday, March 17, 2015

    MTOTO WA MCHEZAJI YANGA AWA MSEMAJI WA KLABU YA SIMBA

    Hajji Sunday katika 'gwanda' la CCM 
    MTOTO wa mchezaji wa zamani wa Yanga SC, Sunday Manara ‘Computer’, aitwaye Hajji Sundy ameteuliwa kuwa Msemaji ya klabu ya Simba SC.
    Taarifa ya Simba SC iliyotolewa leo, imesema kwamba aliyekuwa Msemaji wa klabu hiyo, Humphrey Nyasio sasa atatafutiwa nafasi nyingine ya kazi katika klabu hiyo.
    Pamoja na kwamba baba yake amecheza Yanga na ni mpenzi wa klabu hiyo pia, lakini Hajji ametokea kuwa mpenzi wa Simba SC tangu angali mdogo.
    Hajji mwenye ulemavu wa ngozi, maarufu kama albino amewahi kufanya kazi katika vyombo mbalimbali vya Habari Tanzania na pia ni mmoja wa makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM). 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTOTO WA MCHEZAJI YANGA AWA MSEMAJI WA KLABU YA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top