• HABARI MPYA

    Tuesday, March 17, 2015

    MAHAKAMA YARUHUSU LIGI MBILI KENYA

    Na Vincent Malouda, NAIROBI
    KURUHUSIWA kwa kampuni inayosimamia ligi kuu Kenya, KPL, kuendelea na ligi yake kunaashiria ligi mbili kuu nchini Kenya.
    Hii ni baada ya hakimu wa Mahakama kuu ya Kenya, Roselyn Ekirapa Aburili kutupilia mbali marufuku ya KPL kutoanda ngarambe zozote kwa mujibu wa maombi yaliyowasilishwa mahakamani na Shirikisho la Soka Kenya, FKF, ambalo halikutaka kampuni hiyo kusimamia ligi kuu msimu huu baada ya kutoelewana kuhusu idadi ya timu zitakazoshiriki ligi kuu.
    Kutokana na hayo, FKF ilianzisha ligi yake kuu huku KPL ikisimamisha mechi zake majuma matatu yaliyopita kufuatia amri ya korti licha ya kucheza mechi za ufunguzi Februari 21 na 22.
    Kwa majuma matatu sasa timu kumi na nne zikiwemo Gor Mahia ambao ni mabingwa watetezi hazijashiriki pambano lolote la ligi kuu zikisubiri uamuzi wa mahakama ambapo jaji Aburili aliwapa mashabiki wa soka kitu wanachopenda moyoni mchana wa leo.
    Sasa ni rasmi ya kwamba ligi kuu itaendelea tangia ino Jumatano Nakuru AllStars wakiandaa zulia la Afraha kudananadana na Sofapaka kisha siku ya Alhamisi, Gor Mahia washikane mashati na Bandari ugani City.
    Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya wataanza kutetea taji lao dhidi yao ya Chemelil Sugar Jumapili
     

    RATIBA YA MECHI ZA WIKIENDI HII LIGI KUU KENYA 

    Jumamosi
    Thika United Vs Mathare United – Thika
    Ulinzi Stars Vs Western Stima – Afraha
    KCB Vs Nakuru AllStars – City Stadium
    SoNy Sugar Vs Muhoroni Youth – Awendo
    Nairobi City Stars Vs AFC Leopards – Nyayo
    Jumapili
    Sofapaka Vs Bandari – Machakos
    Tusker Vs Ushuru – Nyayo
    Gor Mahia Vs Chemelil Sugar - Nyayo
    Haya yanajiri huku ligi ya FKF ya timu kumi 18 ikishika moto. 
    Kufikia sasa Shabana FC wanaongoza jedwali kwa pointi 
    tisa, mbili zaidi ya Zoo Kericho na  Kakamega Homeboyz 
    wanaoshikilia nafasi za pili na tatu mtawalia huku Moyas, 
    Kariobangi Sharks na Nakumatt wakiburura manyoya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAHAKAMA YARUHUSU LIGI MBILI KENYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top