• HABARI MPYA

    Tuesday, April 10, 2012

    SAMATTA, ULIMWENGU MATAWI YA JUU TP MAZEMBE

    Pichani, washambuliaji chipukizi wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta wa pili kulia na Thomas Emmanuel Ulimwengu wa pili kushoto wakimkabidhi Idriss Mbuyamba katikati yao, zawadi ya shindano linalondeshwa na klabu yao, Tout Puissant Mazembe la ‘Picha ya Wa Zamani’ Jumamosi mjini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mbuyamba alimwaga machozi kwa sababu ya Samatta, kutokana na kutoamini macho yake baada ya kukutana na staa huyo, baada ya kushinda shindano hilo. Sama Goal atarajea uwanjani wii hii, baada ya kupona bega aliloumia kwenye mechi ya kwanza ya TP Mazembe dhidi ya Power Dynamos y Zambia mjini Kitwe iliyoisha kwa sare ya 1-1. Mazembe iliitoa Dynamos kwa jumla ya mabao 7-1, baada ya kuifunga 6-0 katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 32 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki. Samatta ndiye aliyefunga bao katika sare ya 1-1 mjini Kitwe.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA, ULIMWENGU MATAWI YA JUU TP MAZEMBE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top