• HABARI MPYA

    Wednesday, April 11, 2012

    LIVERPOOL YAONA MWEZI

    Wachezaji wa Liverpool wakimpongeza Andy Carroll
    BLACKBURN, England
    MSHAMBULIAJI Andy Carroll alifunga bao kwa kichwa katika dakika ya kwanza ya dakika za majeruhi na kuiwezesha Liverpool kushinda 3-2 dhidi ya Blackburn iliyo hatarini kushuka daraja.
    Lakini Liverpool ilimpoteza wake mwingine, aliyesimamishwa kuelekea Nusu Fainali ya Kombe la FA mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Everton.
    Mabao ya Maxi Rodriguez dakika ya 13 na 16 yaliwafanya Wekundu wa Anfield waongoze 2-0.
    Kipa wa Liverpool, Alexander Doni, aliyechukua nafasi ya Pepe Reina anayetumikia adhabu, alipewa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumuangusha Junior Hoilett kwenye eneo la hatari dakika ya 25.
    Kipa aliyetokea benchi, Brad Jones alizuia mkwaju wa penalti wa Ayegbeni Yakubu dakika ya 27, lakini Yakubu akafunga mabao mawili dakika za 36 na 61 na kufanya 2-1.
    Penalti aliyopiga baadaye ilimfanya atomize mabao 16.
    Jones alikuwa mwenye bahati kwa kutotolewa nje kwa kadi nyekundu, baada ya kumsukuma Yakubu kwenye eneo la hatari.
    Liverpool ni ya nane sasa kwa pointi zake 46, wakati Blackburn ni ya 18 nyuma ya Queens Park Rangers kwa tofauti ya mabao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAONA MWEZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top