• HABARI MPYA

    Sunday, April 22, 2012

    INIESTA: REAL WAMETUPIGA MKUKI WA MOYO, LAKINI CHELSEA WATAITA MAJI MMA JUMANNE


    Iniesta akiwa haamini macho yake

    KIUNGO wa Barcelona, Andres Iniesta amesema kwamba kipigo cha jana katika Clasico kimewaumiza sana mioyo yao, lakini ameahidi vijana wa Pep Guardiola wataibuka katika mechi ya marudiano ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Chelsea.
    Wakatalunya hao waliingia kwenye mchezo huo kwa matumaini ya kupunguza pengo la idadi ya pointi wanazozidiwa na Los Blancos kileleni mwa La Liga na kubaki moja, lakini sasa wanaachwa pointi saba baada ya kulala 2-1 Camp Nou, Cristiano Ronaldo akiifungia bao la ushindi timu yake dakika ya 73, dakika tatu tangu Alexis Sanchez aisawazishie Barca, kufuatia Sami Khedira kufunga la kuongoza mapema.
    Real sasa wanahitaji sare moja na kushinda mechi moja katika mechi nne zilizobaki ili kutangaza ubingwa na hata Iniesta amesema anafikiri mbio za ubingwa sasa zimkwisha Hispania.
    “Imetuumiza miyo yetu kutokuwa tena kwenye mbio za taji la La Liga, lakini tukubali,” alisema kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania na kuongeza; “Taji la La Liga dhahiri limetuponyoka. Tofauti ni kubwa kwenye pointi na mechi zilizobaki ni chache.
    "Tulijua itakuwa ngumu, hususan kutokana na kutambua kwamba wanajitegemea wao wenyewe – lakini tumeacha liende.
    “Suluhisho pekee kwetu lilikuwa ni ushindi, na walicheza na hilo akilini mwao. Kwa sare, wakati ilipoonekana kuwa ngumu, tulipigania ushindi, walitumaliza haraka sana.”
    Iniesta, pamoja na hayo hana shaka Barca itasahau kuhusu kipigo cha Clasico na kuingia vitani tena kujaribu kuupiku ushindi wa 1-0 wa Chelsea kwenye mchezo wa kwanza kwao.
    "Tunatakiwa tujiandae na tuwe sawa kwa ajili ya mechi ya Jumanne," alisema mshindi huyo wa Kombe la Dunia.
    "Tunataka kuelekeza fikra zetu katika mashindano mengine. Maji yakishamwagika, hayazoleki.
    Ni mchezo tofuti kabisa dhidi ya Chelsea. Kipi tunafikiria ni kuhusu kuingia Fainali ya Ligi ya Mabigwa.”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: INIESTA: REAL WAMETUPIGA MKUKI WA MOYO, LAKINI CHELSEA WATAITA MAJI MMA JUMANNE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top