• HABARI MPYA

    Sunday, April 22, 2012

    MUAMBA AZUNGUMZIA AFYA YAKE, ASEMA ANGEKUWA TAAHIRA


    Muamba katikati baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalik

    KIUNGO wa Bolton, Fabrice Muamba, amezungumza kwa mara ya kwanza tangu apate matatizo ya moyo katika mechi, akisema; “Niko hai sana.'' Alisema katika taarifa iliyoifikia
    bongostaz.blogspot.com.
    Mapigo ya moyo ya Muamba yalisimama kwa dakika 78 mwezi uliopita katika Robo Fainali ya Kombe la  FA dhidi ya Tottenham, lakini na kutoka hospitali mapema wiki hii.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, Muamba amesema leo na kunukuliwa na gazeti la The Sun la Uingereza kwamba, 'hakusikia maumivu kabisa'' kabla ya kuzimia, zaidi ya kuanza kusikia kizunguzungu.
    Alisema: ''Nilihisi nalegea na mwili kupoteza nguvu kabla ya kuanguka, kichwa changu kikiangukia uwanjani mbele yangu, kasha ndivyo ikawa hivi. Giza, hakuna kitu.''
    Muamba alisema 'kwa dakika 78 nilikuwa mfu na hata kama nimepona, ilitarajiwa nitakuwa na matatizo ya ubongo, lakini niko hai sana.'
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MUAMBA AZUNGUMZIA AFYA YAKE, ASEMA ANGEKUWA TAAHIRA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top