• HABARI MPYA

    Saturday, April 11, 2009

    TFF WAKUTANA LEO, MGOSI ATAPONA?


    WAKATI Ligi Kuu ya Tanzania bara inaelekea ukingoni, kamati ya mashindano itakutana leo kujadili mwenendo mzima wa ligi ikiwa ni pamoja na mchezaji Musa Hassan Mgosi na timu ya Kagera Sugar ambayo inamaliza ligi bila ya kuwa na timu ya vijana.
    Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema suala la Kagera Sugar kupuuza kanuni ya kuwa na timu ya vijana ikiwa ni klabu pekee ambayo inamaliza ligi bila ya kuwa na timu ya vijana.
    Katika moja ya kanuni za ligi ni lazima timu ziwe na timu za vijana na timu ambayo haijafanya hivyo inachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kushushwa daraja.
    Mbali na Kagera pia kamati hiyo itawajadili mchezaji wa Simba Mussa Mgosi na Shaaban Kado wa Mtibwa Sugar ambao walifungiwa kucheza michezo miwili, adhabu ambayo walishaimaliza.
    Wachezaji hao walifungiwa michezo miwili baada ya kupigana wakati Simba ikicheza na Mtibwa mjini Morogoro hivi karibuni na Simba kukubali kipigo cha bao 1-0.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF WAKUTANA LEO, MGOSI ATAPONA? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top