WENYEJI, Coastal Unión wamelazimishwa sare ya bila mabao na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Kwa matokeo hayo, Coastal Unión inafikisha pointi 34 ingawa inabaki nafasi ya nne, wakati Tanzania Prisons inafikisha pointi 32 nayo inabaki nafasi ya sita baada ya wote kucheza mechi 25.
0 comments:
Post a Comment