• HABARI MPYA

    Tuesday, August 04, 2015

    WAKASO AMFUATA MUNTARI UARABUNI BAADA YA MAMBO KWENDA MRAMA ULAYA

    KIUNGO wa kimataifa wa Ghana, Mubarak Wakaso (pichani) amekamilisha uhamisho wake kwenda Al-Ittihad ya Saudi Arabia kwa Mkataba wa miaka mitatu.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amefaulu vipimo vya afya jana mjini Milan na mara moja atajiunga na wachezaji wenzake wapya mwishoni mwa wiki.
    Wakaso alikuwa katika wakati mgumu katika Ligi ya Urusi kabla ya kwenda kwa mkopo Celtic ya Ligi Kuu ya Scotland msimu uliopita, ambako pia alishindwa kung’ara licha ya kuwa na mwanzo mzuri.
    Na Wakaso ametua katika timu hiyo baadab ya kusukiwa mipango na mchezaji mwenzake wa kimataifa wa Ghanam Sulley Muntari, ambaye awali alimpendekeza Kevin-Prince Boateng anayechezwa Schalke 04 kwa sasa lakini akakataa kuondoka Ujerumani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAKASO AMFUATA MUNTARI UARABUNI BAADA YA MAMBO KWENDA MRAMA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top