• HABARI MPYA

    Sunday, August 02, 2015

    ARSENAL WAIKALISHA CHELSEA MECHI YA NGAO 1-0 WEMBLEY

    Wachezaji wa Arsenal wakisherehekea ushindi wao wa Ngao ya Jamii leo baada ya kuifunga Chelsea 1-0 PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    KOCHA Mfaransa Arsene Wenger amevunja ‘uteja’ wake kwa Mreno, Jose Mourinho leo. Wenger ameshinda mechi ya kwanza dhidi ya Mourinho katika mechi 14, baada ya kuiwezesha Arsenal kutwaa Ngao ya Jamii England kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Chelsea Uwanja wa Wembley, London.
    Hilo ni taji la pili ndani ya miezi mitatu kwa Arsenal, baada ya miezi miwili na ushei iliyopita kutwaa Kombe la FA katika fainali iliyopigwa uwanja huo huo.
    Kipa wa zamani wa Chelsea, Petr Cech alidaka kwa ustadi mkubwa huku bao pekee la Arsenal likifungwa na kiungo Alex Oxlade-Chamberlain dakika ya 24.
    Kikosi cha Arsenal kilikuwa; Cech, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Ramsey, Oxlade-Chamberlain/Arteta dk77, Cazorla, Ozil/Gibbs dk82 na Walcott/Giroud dk66.
    Chelsea: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry/Moses dk82, Azpilicueta/Zouma dk69, Matic, Ramires/Oscar dk54, Willian, Fabregas, Hazard na Remy/Falcao dk45. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL WAIKALISHA CHELSEA MECHI YA NGAO 1-0 WEMBLEY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top