• HABARI MPYA

    Tuesday, April 10, 2012

    RAIS FIFA SASA ALHAMDULILLAH

    Havelange
    MADAKTARI wamesema rais wa zamani wa FIFA, Joao Havelange anaendelea vizuri baada ya kupatiwa tiba makini ya matatizo ya moyo, kufuatia kurejeshwa chumba cha wagongwa wanaostahili uangalizi makini katika hospitali anayotibiwa nchini Brazil.
    Madaktari wamesema babu huyo wa umri wa miaka 95, Havelange ianapata nafuu kutoka matatizo yake ya moyo ambayo yalimfanya awe taabani katika hospitali ya Samaritano, ambako alilazwa kwa zaidi ya wiki tatu baada ya athari zilizogundulika katika kifundo cha mguu wake wa kulia.
    Dk. Joao Mansur Filho amesema Havelange atakuwa sawa haraka iwezekanavyo.
    Havelange alikuwa rais FIFA kuanzia 1974-1998. Alistaafu katika kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC) mwishoni mwa mwaka jana kwa sababu za kiafya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAIS FIFA SASA ALHAMDULILLAH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top