KIUNGO mshambuliaji wa Kimataifa wa Burkina Faso, Stephane Aziz Ki wa Yanga ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kwa mwezi Aprili, huku Muargentina Miguel Ángel Gamondi wa timu hiyo pia akishinda Tuzo ya Kocha Bora mwezi huo.
Wakati Aziz Ki amewashinda mchezaji mwenzake wa Yanga, Joseph Gnadou Guede alioingia nao Fainali - Gamondi amewashinda Mfaransa Bruno Ferry wa Azam FC na mzawa, Malale Hamsini wa JKT Tanzania alioingia nao Fainali pia.
0 comments:
Post a Comment