• HABARI MPYA

    Saturday, May 15, 2021

    SIMBA YACHAPWA 4-0 JOHANNESBURG NA KAIZER CHIEFS ROBO FAINALI YA KWANZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

     TIMU ya Simba SC imechapwa mabao 4-0 na wenyeji, Kaizer Chiefs katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika leo Uwanja wa FNB Jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
    Mabao ya Kaizer Chiefs yamefungwa na Eric Molomowanadou Mathoho dakika ya sita, Samir Nurkovic dakika ya 34 na 57 na David Leonardo Castro Cortés dakika ya 63.
    Sasa Simba SC watatakiwa kushinda 5-0 katika mchezo wa marudiano Jumamosi ya wiki ijayo ili kwenda Nusu Fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1975.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA YACHAPWA 4-0 JOHANNESBURG NA KAIZER CHIEFS ROBO FAINALI YA KWANZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top