MABAO ya Sergio Aguero dakika ya 57 na Ferran Torres dakika ya 59 jana yaliipa Manchester City ushindi wa 2-0 dhidi ya Crystal Palace kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Selhurst Park Jijini London.
Sasa Manchester City imefikisha pointi 80 baada ya kucheza mechi 34 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi 13 zaidi ya Manchester United ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.
0 comments:
Post a Comment