• HABARI MPYA

    Wednesday, May 05, 2021

    JKT TANZANIA YAILAZA NAMUNGO FC 1-0 NA KUJIONDOA KWENYE ENEO LA HATARI LIGI KUU BARA

     JKT Tanzania imeichapa Namungo FC 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
    Bao pekee la JKT leo limefungwa na Daniel Mecha dakika ya tano ya mchezo huo na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 30 baada ya kucheza mechi 27 na kupanda hadi nafasi ya 14 kutoka ya 17 kwenye ligi ya timu 18, wakati Namungo FC inabaki na pointi zake 31 za mechi 23 katika nafasi ya 11.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JKT TANZANIA YAILAZA NAMUNGO FC 1-0 NA KUJIONDOA KWENYE ENEO LA HATARI LIGI KUU BARA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top