Wachezaji wa timu ya wasichana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite wakifuraha baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Uganda jioni ya leo Uwanja wa Star Times mjini Kampala kwenye mchezo wa marudiano kuwania tiketi za fainali za Kombe la Dunia za U20 Costa Rica na Panama. Tanzanite imeshinda 2-1, mabao yake yakifungwa na Diana Msewa dakika ya 59 na Opa Clement dakika ya 68, baada ya Phiona Nabbumba kuanza kuwafungia wenyeji dakika ya 48. Tanzania inasonga mbela kwa ushindi wa jumla wa 4-2 kufuata kushinda 2-1 pia nyumbani mwezi uliopita na sasa itamenyana na mshindi wa jumla kati ya Sierra Leone na Senegal, mechi ya kwanza Machi 20 ugenini na marudiano Machi 27 nyumbani.
Puka Nacua puts antisemitic controversy behind him with touchdown on
Thursday Night Football... and there's no sign of THAT celebration
-
The Rams superstar sparked fury on a livestream with Adin Ross and N3on
earlier in the week, in which he devised a touchdown dance which included
an offens...
36 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment