• HABARI MPYA

    Wednesday, December 10, 2025

    BARCELONA WATOKA NYUMA NA KUSHINDA 2-1 DHIDI YA EINTRACHT FRANKFURT


    WENYEJI, FC Barcelona jana walitoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya Eintracht Frankfurt katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Spotify Camp Nou Jijini Barcelona, Hispania.
    Eintracht Frankfurt walitangulia kwa bao la winga wa kulia, Ansgar Knauff dakika ya 21, kabla ya beki wa kulia Mfaransa Jules Olivier Koundé mwenye asili ya Benin kuifungia mfululizo Barcelona dakika ya 50 na 53.
    Kwa ushindi huo, Barca inafikisha pointi 10 na kusogea nafasi ya 14 kwenye ya timu 36 za Ulaya, wakati Eintracht Frankfurt inabaki na pointi zake nne nafasi ya 30 baada ya timu zote kucheza mechi sita. 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCELONA WATOKA NYUMA NA KUSHINDA 2-1 DHIDI YA EINTRACHT FRANKFURT Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top