• HABARI MPYA

    Wednesday, June 18, 2014

    HISPANIA YAVULIWA UBINGWA WA DUNIA NA KUTUPWA NJE YA MICHUANO NA CHILE

    AIBU gani hii! Hispania imevuliwa ubingwa wa dunia usiku huu baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Chile katika mchezo wa Kundi B Uwanja wa Maracana, Rio de Jeneiro, Brazil.
    Maana yake, Hispania watacheza mechi ya kukamilisha ratiba dhidi ya Australia kisha kurejea nyumbani mapema, wakiiacha michuano bado mibichi kabisa.  
    Mabao yaliyoizamisha Hispania leo yamefungwa na 
    Eduardo Vargas dakika ya 19 na Charles Aranguiz dakika ya 43 - hivyo ukijumlisha na kipigo cha 5-1 walichopewa na Uholanzi maana yake hawana maisha tena katika Fainali za Brazi 2014.
    Uholanzi na Chile zote zina pointi sita kila moja, wakati Australia na Hispania hazina pointi. Kwa Chile ushindi wa leo ni sawa na kulipa kisasa cha kufungwa 2-1 nchini Afrika Kusini mwaka 2010 katika mchezo wa mwisho wa kundi kwenye michuano hiyo.
    Mwanzo mzuri: Eduardo Vargas akishangilia baada ya kuifungia Chile bao la kwanza dhidi ya Hispania

    Kocha Vicente Del Bosque atajutia uamuzi wa kuendelea kumpanga kipa Iker Casillas, kwani kwa mara nyingine leo amefungwa mabao ya ‘kibwege’. 
    Kikosi cha Hispania kilikuwa; Casillas, Azpilicueta, Martinez, Ramos, Alba, Busquets, Alonso/Koke dk46, Silva, Iniesta, Pedro/Cazorla dk77 na Costa/Torres dk64.
    Chile; Bravo, Medel, Silva, Jara, Isla, Aranguiz/Gutierrez dk64, Diaz, Mena, Vidal/Carmona dk88, Vargas/Valdivia dk85 na Sanchez.
    Unconventional: Vargas fell to the floor while beating Iker Casillas in the Spanish net
    Amekwisha: Vargas akimtungua kiulaini kipa aliyechuja Iker Casillas
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HISPANIA YAVULIWA UBINGWA WA DUNIA NA KUTUPWA NJE YA MICHUANO NA CHILE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top