• HABARI MPYA

    Wednesday, June 13, 2012

    SIMBA, YANGA NA AZAM ZAMGOMBEA DAMAYO


    Damayo

    KLABU za Simba, Yanga na Azam tangu juzi zinapigana vikumbo kuwania saini ya kiungo mkabaji wa JKT Ruvu, chipukizi Frank Damayo na hadi sasa hakuna timu ambayo imefanikiwa kuinasa.
    BIN ZUBEIRY imezungumza na Damayo mwenyewe amesema ni kweli timu zote hizo na nyingine mbili, Mtibwa Sugar na Coastal Union zinamfuatilia ila hadi hadi saa 5:00 usiku alikuwa hajasaini timu yoyote.
    Damayo alisema timu inayomtaka kwanza lazima izungumze na klabu yake na maelekezo atakayopewa na mwajiri wake ndiyo atakayoyafuata.
    Damayo amekuwa lulu ghafa, baada ya kucheza soka ya kuvutia katika mchezo wa Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunai Jumapili kati ya Tanzania na Gambia.
    Katika mechi hiyo ambayo Taifa Stars iliwatungua Nge wa Gambia 2-1, Damayo alicheza kwa uelewano mkubwa na Kelvin Yondan na kiungo wa juu, Mwinyi Kazimoto, wote wachezaji wa Simba.
    Yondan amesaini Yanga, ingawa na klabu yake, Simba SC ambayo pia anachezea Mwinyi Kazimoto aliyetokea JKT Ruvu pia inadai ina mkataba naye na sasa hatima yake itategemea makubaliano baina ya klabu hizo mbili zinazomgombea.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA, YANGA NA AZAM ZAMGOMBEA DAMAYO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top