| Mgombea nafasi ya Ujumbe katika uchaguzi wa Simba SC mwezi ujao, Juma Abbas Pinto akiwa na kipa wa Manchester United, David de Gea baada ya kukutana naye jana mjini Lisbon, Ureno. Pinto, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) alikuwa Ureno kutazama fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana baina ya Real Madrid na Atletico Madrid, wakati de Gea yupo nchini humo na timu ya taifa ya Hispania iliyoweka kambi ya kujiandaa na Kombe la Dunia mwezi ujao Brazil. |
0 comments:
Post a Comment