• HABARI MPYA

    Wednesday, June 13, 2012

    MZEE MWINYI MGENI RASMI TUZO ZA WANAMICHEZO BORA TZ KESHO


    Mwenyekiti wa TASWA, Juma Abbas Pinto katikati akizungumza na Waandishi wa Habari mchana huu, kulia Katibu wake Amir Ally Mhando na kushoto ni Meneja Mawasiliano wa SBL, Imani Lwinga.

    RAIS mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ally Hassan Mwinyi, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za utoaji wa tuzo za wanamichezo bora Tanzania kesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
    Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Abbas Pinto amesema katika Mkutano na Waandishi wa Habari mchana huu, ukumbi wa City Sports Lounge, Mtaa wa Samora, Dar es Salaam kwamba, wamemchangua Mwinyi kwa sababu alikuwa ana mchango mkubwa katika sekta ya michezo enzi zake, akiwa Ikulu tangu 1985 hadi 1995 alipomuachia Benjamin William Mkapa.
    Pinto amesema kwamba maandalizi ya sherehe hizo yamekamilika na anawashukuru sana wadhamini wa tuzo hizo, Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kwa mchango wao mkubwa.
    Katika tuzo hizo, kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Fadhil Hakizimana Niyonzima wa Yanga, atachuana na Kipre Tchetche wa Ivory Coast anayechezea Azam FC na Mganda Emmanuel Okwi wa Simba kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa mwaka wa kigeni.
    Kwa upande wa wanasoka wazalendo, tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka inawaniwa na John Bocco, Aggrey Morris, wote wa Azam na Juma Kaseja wa Simba, wakati kwa wachezaji wa Tanzania wanaocheza nje wanaoshindana ni Henry Joseph wa Kongsvinger ya Norway na Mbwana Samatta wa Tout Puissant Mazembe ya DRC.
    Kwa upande wa wanawake, Sophia Mwasikili anayecheza Uturuki, anashindana na Asha Rashid ‘Mwalala’, Mwanahamisi Omary wote wa Mburahati Queens, Fatuma Mustapha wa Sayari na Eto’o Mlenzi wa JKT.


    ORODHA KAMILI YA WANAOWANIA TUZO:
    KIKAPU:
    WANAWAKE
    DORITHA  MBUNDA :-JKT QUEENS
    EVODIA  KAZINJA:-JKT QUEENS
    FARAJA MALAKI:-JESHI STARS
    WANAUME
    ALPHA KISUSI-Vijana
    FILBERT MWAIPUNGU:-ABC
    GILBERT BATUNGI:-ABC
    NETIBOLI:
    LILIAN SYLIDION
     DORITHA MBUNDA
     GOFU
    WANAWAKE:
    Madina Iddi (Umri miaka 27)
    Hawa Wanyeche (Umri miaka 26)
    Ayne Magombe (Umri miaka 24)

    WANAUME:
    Frank Roman
    Nuru Mollel
    Issac Anania
    GOFU WA KULIPWA:
    FADHILI  SAIDI NKYA.
    YASINI SALEHE
    HASSANI KADIO

    OLIMPIKI MAALUM
    Ahmada Bakar
    Amina Daud Simba-kisahani na tufe
    Othman Ally Othman-mkuki, kisahani na tufe.
    Cio..
    PARALIMPIKI
    WANAUME
    ZAHARANI MWENEMTI
    JOSEPH NZIKU
    YOHANA MWILA
    WANAWAKE
    FAUDHIA CHAFUMBWE
    SIWEMA KILYENYI
    JANETH MADISE
    NGUMI ZA RIDHAA
    SULEIMAN SALUM KIDUNDA
    VICTOR NJAITI
    ABDALAH KASSIM
    CIO…

    WAOGELEAJI
    (WANAWAKE)
    MAGDALENA MOSHI
    GOURI KOTECHA
    MARIAM FOUM

    WANAUME
    AMMAAR GHADIYALI
    OMARI ABDALLAH

    JUDO...
     MBAROUK SELEMANI MBAROUK
    UNDER 81KG MEN JUDO PLAYER
     MOHAMED KHAMIS JUMA
    OVER 90KG MEN JUDO PLAYER
     AZZAN HUSSEIN KHAMIS
    UNDER 60KG Judo player

    CIO…
    WAVU…

    WANAWAKE
    ZUHURA HASSAN-JESHI STARS
    THERESIA Ojode -JESHI STARS DAR
    EVERLYNE ALBERT- MAGEREZA
    WANAUME
    MBWANA ALLY- MZINGA CORPORATION  - MOROGORO
    KEVIN PETER -MAGEREZA – DAR
    FARHAN ABUBAKAR- MAFUNZO ZNZ
    CIO…
    NGUMI ZA KULIPWA
    Benson Mwakyembe
    Nasibu Ramadhan
    Francis Cheka
    Nassib Ramadhan
    Fadhil Majia

    TENISI:
    WANAUME
    WAZIRI SALUMU
     OMARY ABDALAH
    HASSANI KASSIMU

    WANAWAKE
    REHEMA ATHUMANI
     MKUNDE IDDY
    VIOLET PETER
    Cio…

    BAISKELI
    Wanawake
    Sophia Hussein
    Sophia Anderson
    WANAUME:
    Richard Laizer
    Hamisi Hussein

    WACHEZAJI WA TANZANIA WANAOCHEZA NJE
    Henry Joseph-Soka
    Mbwana Samatta-Soka
    Sophia Mwasikili-Soka
    MCHEZAJI BORA CHIPUKIZI
    Theresia Ojode- wavu (Jeshi Stars)
    SHOMARI KAPOMBE- (soka) SIMBA
    Salum Abubakari-Azam (soka)
    MCHEZAJI WA NJE ANAYECHEZA TANZANIA
    Haruna Niyonzima-Yanga (soka)
    Kipre Tchetche-Azam (soka)
    Emmanuel Okwi-Simba (soka).

    SOKA (WANAWAKE)
    Asha Rashid-Mburahati Queens
    Mwanahamisi Omary-Mburahati Queens
    Fatuma Mustapha-Sayari
    Ito Mlenzi-JKT

    WANAUME
    John Bocco-Azam
    Aggrey Morris-Azam
    Juma Kaseja-Simba
    RIADHA
    WANAWAKE
    Zakia Mrisho
    Mary Naali
    Jaqueline Sakila

    WANAUME
    Dickson Marwa
    Alphonce Felix

    MIKONO
    WANAWAKE
    Abinery Kusencha-JKT Ruvu
    Kazad Mtong-Magereza Kiwira
    Faraji Shaibu  Khamis-Nyuki Zbar
    WANAUME:
    Doris Mangara-Magereza Kiwira
    Zakia Seif-Ngome Dar
    Mary Kimiti-Magereza Kiwira.
    Cio…
    KRIKETI
    WANAWAKE
    MoniCa Pascal
    Asha Daudi
    Esther Wallace

    WANAUME
    Kassimu Nassoro
    Benson Mwita
    Riziki Kiseto
    TUZO YA HESHIMA-ITATANGAZWA SIKU HIYO
    MWANAMICHEZO BORA WA TANZANIA 2011-ATAPATIKANA MIONGONI MWA WASHINDI WA KILA MCHEZO.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MZEE MWINYI MGENI RASMI TUZO ZA WANAMICHEZO BORA TZ KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top