• HABARI MPYA

    Wednesday, September 03, 2014

    KLABU ENGLAND ZIMEFANYA KUFURU MBAYA USAJILI HUU, LA LIGA, SERIE A, BUNDESLIGA ZOTE TUPWA HUKO

    KLABU za Ligi Kuu ya England zimetumia Pauni Milioni 858 baada ya dirisha la usajili msimu huu kufungwa, ambayo ni zaidi ya kiasi kilichotumika kwa klabu za La Liga ya Hispania (Pauni Milioni 425), Serie A ya Italia (Pauni Milioni 260) na Ligue 1 ya Ufaransa (Pauni Milioni 100) jumla.
    Hii imeipiku hata Ujerumani ambako klabu zilipoamua kuingia sokoni kwa fujo Bundesliga zilitumia Pauni Milioni 250 jumla pamoja na Pauni Milioni 100 kwa awamu moja ya usajili.
    Sehemu kubwa ya fedha inatokana na mikataba ya Televisheni England ambayo inazipa jeuri klabu kusajili kwa bei kubwa na kulipa mishahara minono wachezaji. 
    Am I worth it? Angel di Maria was the most expensive acquisition after joining United for a record £59.7m
    Mimi ni bosi wao? Angel di Maria amekuwa mchezaji aliyenunuliwa kwa bei mbaya zaidi kihistoria Uingereza baada ya Manchester United kulipa Pauni Milioni 59.7 Real Madrid

    Chati hii inaonyesha namna klabu zilivytumia fedha kusajili Ulaya, Ligi Kuu England ikiongoza kwa kutumia Pauni Milioni 857.68

    FEDHA NYINGI ZIMEKWENDA KWA WACHEZAJI WA KIGENI
    Katika kiasi hicho cha jumla cha fedha, klabu za Ligi Kuu ya England zimetumia Pauni Milioni 520.8 kusajili wachezaji wa kigeni, yaani kutoka née ya Uingereza  (England, Scotland and Wales). 

    DILI ZA BEI CHAFU ZAIDI USAJILI HUU ENGLAND

    Angel Di Maria [Real Madrid - Manchester United] Pauni Milioni 59.7
    Alexis Sanchez [Barcelona - Arsenal] Pauni Milioni 35
    Diego Costa [Atletico Madrid - Chelsea] Pauni Milioni 32
    Eliaquim Mangala [FC Porto - Manchester City] Pauni Milioni 32
    Cesc Fabregas [Barcelona - Chelsea] Pauni Milioni 30
    Ander Herrera [Athletic Bilbao - Manchester United] Pauni Milioni 29
    Romelu Lukaku [Chelsea - Everton] Pauni Milioni 28
    Luke Shaw [Southampton - Manchester United] Pauni Milioni 27 (inaweza kupanda hadi Milioni 31)
    Adam Lallana [Southampton - Liverpool] Pauni Milioni 25
    Dejan Lovren [Southampton - Liverpool] Pauni Milioni 20
    Lazar Markovic [Benfica - Liverpool] Pauni Milioni 20
    City slicker: Eliquiam Managal arrived from Porto for £32m
    Top Gun: Alexis Sanchez was the second costliest transfer for £35m
    Dau kubwa: Usajili wa Eliquiam Mangala (City) na Alexis Sanchez (Arsenal) ump kwenye rekodi ya usajili wa bei mbaya
    Blues brother: Cesc Fabregas joined Chelsea from Barcelona
    Super striker: Jose Mourinho brought in Diego Costa early
    Pacha wa Blues: Chelsea imefanya biashara ya maana kuwasajili Cesc Fabregas (kushoto) na Diego Costa (kulia)

    KLABU IPI IMEFANYA USAJILI BORA?
    Manchester United imetumia (jumla ya Pauni Milioni 153.1), na Stoke imetumia (Pauni Milioni 3.4) wakati Southampton imetengeneza faida ya Pauni Milioni 30.7 katika usajili wake.
    Chelsea imefanya biashara nzuri yenye thamani halisi ya vipengele vya fedha, ikitengeneza faida na kuboresha timu. Na Leicester na Southampton pia zimefanya vizuri katika thamani halisi kwa kutengeneza timu nzuri kwa gharama kidogo.
    Wachezaji walionunuliwa ni pamoja na makipa saba, mabeki 36, viungo 37 na washambuliaji 23.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KLABU ENGLAND ZIMEFANYA KUFURU MBAYA USAJILI HUU, LA LIGA, SERIE A, BUNDESLIGA ZOTE TUPWA HUKO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top