“MARINE”    
“SAFINA”
“NGANO
“UNGA
“UNGA
“WATER”
HABARI MOTOMOTOHABARI MOTOMOTOHABARI ZA AFRIKA

KOMBE JIPYA LA LIGI YA MABINGWA AFRIKA NI HILI HAPA

SHIRIKISHO la Soka la Afrika (CAF) kwa kushirikiana na wadhamini wake wakuu, TotalEnergies jana lilizindua Kombe jipya la Ligi ya Mabingwa ya CAF kuashiria ukurasa mpya wa hadhi wa mashindano ya klabu barani Afrika.
Uzinduzi huo ulifanyika katika Makao Makuu ya TotalEnergies ya Afrika Kusini mjini Johannesburg na kuhudhuriwa na baadhi ya magwiji wa soka barani Afrika akiwemo Lucas Radebe, Teko Modise na Siphiwe Tshabalala pamoja na viongozi kadhaa wa soka barani Afrika.
Aidha, viongozi wa klabu za Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Pyramids ya Misri zitakazomenyana katika Fainali ya mwaka huu ya Ligi ya Mabingwa Afrika walihudhuria pia.
“Kulingana na maono ya Rais wa CAF, Dk Patrice Motsepe, tunabadilisha jina na kuweka upya kandanda ya Afrika kwa kuzingatia zaidi mashindano ya klabu kwa sasa,”.
“Taji hili la TotalEnergies CAF Champions League linaonyesha malengo yetu na hatua za ujasiri kuelekea mazingira ya kusisimua ya soka ya klabu barani Afrika. Kwa hili, tunalenga kuinua hadhi ya mashindano ya klabu Afrika ili kuibua vipaji vipya vya soka duniani,” alisema Katibu wa CAF, Véron Mosengo-Omba.
Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika itachezwa Jumamosi ya kesho, Mamelodi Sundowns wakiwa wenyeji wa Pyramids kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa Loftus Versfeld Jijini Pretoria, kabla ya timu hizo kurudiana Juni 1 Uwanja wa Jeshi la Anga wa Juni 30Jijini Cairo, Misri.

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button