HABARI ZA ULAYA
LAMINE YAMAL ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI BORA U-23 LA LIGA

MSHAMBULIAJI chipukizi wa Kimataifa wa Hispania, Lamine Yamal ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu La Liga chini ya umri wa miaka 23.
Yamal ameshinda Tuzo akiwaangusha Fábio Silva, Diego López wa Valencia CF, Jude Bellingham, Arda Güler wote wa Real Madrid, Pedri González anayecheza naye FC Barcelona na Alberto Moleiro wa UD Las Palmas.
Kinara huyo wa mabingwa wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona akiwa ana umri wa miaka 17 tu, amefunga mabao tisa na kutoa pasi za manao 13, ambayo inamfanya awe mchezaji aliyetoa pasi nyingi zaidi za mabao kwenye ubingwa huo.