“SAFINA”
“NGANO
“UNGA
“UNGA
“WATER”
HABARI MOTOMOTOHABARI ZA NYUMBANI

SIMBA SC YAICHAPA SINGIDA BLACK STARS 1-0 NA KUKAA ‘ANGA’ ZA UBINGWA LIGI KUU

WENYEJI, Simba SC wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Steven Dese Mukwala dakika ya 43 akimalizia kazi nzuri ya kiungo Muivory Coast, Jean Charles Ahoua na kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 72, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi moja tu na mabingwa, Yanga baada ya wote kucheza mechi 27.
SIngida Black Stars inabaki na pointi zake 53 nafasi ya nne sasa ikizidiwa pointi nne na Azam FC baada ya wote kucheza mechi 28.
Baada ya mchezo wa leo, timu zote zitasafiri kwenda Babati mkoani Manyara kwa ajili ya mchezo mwingine, Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB Jumapili kuanzia Saa 9:30 Uwanja wa Tanzanite Kwaraa.

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button