“SAFINA”
“NGANO
“UNGA
“UNGA
“WATER”
HABARI ZA AFRIKA

JOSÉ LUIS RIVEIRO NDIYE KOCHA MPYA WA AHLY

KOCHA Mspaniola, José Luis Riveiro jana alitambulishwa kuwa Kocha mpya wa Al Ahly ya Misri wiki mbili tu baada ya kuondoka Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Mara moja Riveiro anapewa jukumu la kwenda kuiongoza Al Ahly katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA inayotarajiwa kufanyika nchini Marekani hivi karibuni.
Ahly, kati ya wawakilishi wenne wa Afrika pamoja na Wydad Athletics ya Morocco, Esparence ya Tunisia na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini – ipo Kundi A pamoja na wenyeji, Inter Miami, Palmeiras ya Brazil na FC Porto ya Ureno.
Washindi wawili wa juu wa kila kundi watakwenda Hatua ya mtoano ya michuano hiyo mipya inayohusisa timu 32.
Ahly ndio klabu yenye mafanikio zaidi barani Afrika na hivi juzi walifanikiwa kutwaa taji la 45 la ubingwa wa Ligi Kuu ya Misri – huku pia wakiwa wameshinda jumla ya mataji 12 ya Ligi ya Mabingwa Afrika ya CAF, manne kati ya hayo wamechukua kuanzia msimu wa 2019-20.
Huu utakuwa ni mmoja kati ya misimu miwili pekee tangu wakati huo ambapo timu nyingine itabeba kombe hilo.
Ahly ilitolewa kwa mabao ya ugenini na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kitoka sare ya 0-0 ugenini na 1-1 nyumbani.
Wapinzani wao kwenye mbio za ubingwa wa Misri msimu huu, Pyramids FC walikwenda Fainali baada ya kuitoa Orlando Pirates kwa kuichapa 3-2 Cairo kufuatia sare ya 0-0 Johannesburg.
Jumapili Pyramids FC watamenyana na Mamelodi Sundowns katika mchezo wa marudiano wa Fainali kuanzia Saa 2:00 usiku Uwanja wa Jeshi la Anga wa Juni 30 jijini Cairo wakitoka kutoa sare ya 1-1 ugenini Uwanja wa Loftus Versfeld Jijini Pretori Mei 24.
Baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa, Al Ahly ilimfuta kazi Kocha Mswisi, Marcel Koller mwishoni mwa mwezi Aprili na Kocha wa Muda, Emad El-Nahhas akaiongoza timu kumalizia msimu na kuiwezesha kutwaa taji la tatu mfululizo la Ligi Kuu.
Riveiro anajiunga na Al Ahly kwa mkataba wa miaka miwili, baada ya kuitumikia Orlando Pirates kwa mafanikio makubwa kwa miaka mitatu akiiwezesha kutwaa mataji matatu ya MTN8 na mawili ya Nedbank Cup mbali na kuifikisha Nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button