“SAFINA”
“NGANO
“UNGA
“UNGA
“WATER”
HABARI MOTOMOTOHABARI ZA KIMATAIFAHABARI ZA ULAYA

BARCELONA WATWAA TAJI LA LIGA KWA MARA YA 28

TIMU ya Barcelona jana imefanikiwa kutwaa taji la Ligi Kuu ya Hispania ‘La Liga’ baada ya ushindi wa ugenini wa mabao 2-0 dhidi ya mahasimu wao wa Katalunya, 0 dhidi ya Espanyol kwenye Uwanja waRCDE, Cornella de Llobregat.

Nyota wa mchezo wa jana alikuwa ni mshambuliaji chipukizi wa umri wa miaka 17, Lamine Yamal Nasraoui Ebana aliyefunga bao la kwanza dakika ya 53 na kutoa pasi ya bao la pili lililofungwa na Fermín López dakika ya 90’+5.
Kwa ushindi huo, Barcelona wanafikisha pointi 85, saba zaidi ya waliokuwa mabingwa watetezi, Real Madrid kuelekea mechi mbili za mwisho kwa wote – hivyo rasmi Blaugrana ni mabingwa wa La Liga kwa mara 28 kihistoria, ikiwa klabu namba kwa mataji mengi ya ligi hiyo baada ya Real Madrid wenye mataji 36.
Pongenzi kwa Kocha Mjerumani, Hansi Flick akiwa katika msimu wake wa kwanza amefanikiwa kurejesha utawala wa Barca Hispania akibeba taji la tatu baada ya Kombe la Mfalme ‘Copa del Rey’ na Super Cup ya Hispania ‘Supercopa de España’.
Mjerumani huyo wa tatu kihistoria kufundisha klabu hiyo baada ya Hennes Weisweiler na Udo Lattek – pia amerejesha ubabe wa Barca kwa Real Madrid baada ya kuwafunga Los Blancos mechi zote nne za msimu zikiwemo mbili zote za La Liga, Fainali ya Super Cup ya Hispañia na Kombe la Mfalme – hii ikiwa mara yaa kwanza katika zama mpya Barca kuwafunga mechi zote za msimu wapinzani wao hao.

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button