• HABARI MPYA

    Tuesday, November 03, 2020

    SAMATTA AISAIDIA FENERBAHCE KUPANDA KILELENI UTURUKI BAADA YA KUICHAPA ANTALYASPOR 2-1

    Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta (kulia) akishangilia na wachezaji wenzake wa Fenerbahce baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Antalyaspor kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Uturuki usiku wa jana Uwanja wa Antalya. 
    Mabao ya Fenerbahce yalifungwa na Ozan Tufan dakika ya 49 na Diego Perotti kwa penalti dakika ya 80 na la Antalyaspor lilifungwa na Lukas Podolski dakika ya 52, wakati Samatta alimpisha Kemal Ademi dakika ya 74. 
    Kwa ushindi huo, Fenerbahce inapanda kileleni ikifikisha pointi 17, moja zaidi ya Antalyaspor baada ya timu zote kucheza mechi saba. 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA AISAIDIA FENERBAHCE KUPANDA KILELENI UTURUKI BAADA YA KUICHAPA ANTALYASPOR 2-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top