TIMU ya taifa ya Equatorial Guinea imefufua matumaini ya kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Libya kwenye mchezo wa Kundi J jana mjini Bata.
Bao pekee la Nzalang Nacional lilifungwa na Ivan Edu Salvador dakika ya 27 na kwa ushindi huo, wanapanda nafasi ya pili wakifikisha pointi sita, wakizidiwa tatu na vinara, Tunisia, wakati Libya inabaki na pointi tatu sawa na Tanzania.
Bao pekee la nyota wa Liverpool, Sadio Mane dakika ya 82 liliipa Senegal ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Guinea-Bissau kwenye mchezo wa Kundi I jana na kuwa timu ya pili kufuzu AFCON ijayo baada ya wenyeji, Cameroon.
Nayo Comoro imeichapa Kenya mabao 2-1 Jijini Moroni katika mchezo wa Kundi G, hivyo kufikisha pointi nane na kuendelea kuongoza kundi hilo katika mbio za Cameroon 2021.
Mabao ya Comoro yalifungwa na El Fardou Ben na Faiz Mattoir, wakati bao pekee la Kenya lilifungwa na Cliff Nyakeya.
Bao pekee la Nzalang Nacional lilifungwa na Ivan Edu Salvador dakika ya 27 na kwa ushindi huo, wanapanda nafasi ya pili wakifikisha pointi sita, wakizidiwa tatu na vinara, Tunisia, wakati Libya inabaki na pointi tatu sawa na Tanzania.
Bao pekee la nyota wa Liverpool, Sadio Mane dakika ya 82 liliipa Senegal ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Guinea-Bissau kwenye mchezo wa Kundi I jana na kuwa timu ya pili kufuzu AFCON ijayo baada ya wenyeji, Cameroon.
Nayo Comoro imeichapa Kenya mabao 2-1 Jijini Moroni katika mchezo wa Kundi G, hivyo kufikisha pointi nane na kuendelea kuongoza kundi hilo katika mbio za Cameroon 2021.
Mabao ya Comoro yalifungwa na El Fardou Ben na Faiz Mattoir, wakati bao pekee la Kenya lilifungwa na Cliff Nyakeya.
MATOKEO MECHI ZOTE ZA JANA KUFUZU AFCON | ||||
---|---|---|---|---|
FT | Burundi | 3 - 1 | Mauritania | View events |
FT | Chad | 1 - 1 | Guinea | View events |
FT | Comoros | 2 - 1 | Kenya | View events |
FT | Guinea-Bissau | 0 - 1 | Senegal | View events |
FT | Equatorial Guinea | 1 - 0 | Libya | View events |
0 comments:
Post a Comment