Mshambuliaji kinda, Ansu Fati akipongezwa baada ya kuifungia Barcelona bao la kwanza dakika ya 11, kabla ya Lucas Olaza kujifunga dakika ya 51 na Sergi Roberto kufunga la tatu dakika ya 90 na ushei katika ushindi wa 3-0 dhidi ya wenyeji, Celta Vigo usiku wa jana kwenye mchezo wa La Liga Uwanja wa Abanca-Balaidos. Pamoja na ushindi huo, kikosi cha Mholanzi, Ronald Koeman kilimaliza pungufu baada ya Clement Lenglet kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 42 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment