SHIRIKISHO la Soka Senegal (FSF) limethibitisha mechi mbili za kirafiki dhidi ya Morocco na jirani zao, Mauritania mwezi ujao.
Simba hao wa Teranga watasafiri kuwafuata Simba wa Atlas, Morocco Jijini Rabat Oktoba 9 kabla ya kuwakaribisha Mauritania siku nne baadaye Jijini Thies.
Mechi hizo zote mbili zitakuwa sehemu ya maandalizi ya mechi za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Cameroon 2021 dhidi ya Djurtus ya Guinea-Bissau.
Kwa mujibu wa FSF, mechi zote zitachezwa bila mashabiki kuingia uwanjani kutokana na hofu ya ugonjwa wa COVID-19.
Senegal inaongoza katika Kundi I ikiwa na poniti sita baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Kongo na 4-1 dhidi ya Eswatini.
Simba hao wa Teranga watasafiri kuwafuata Simba wa Atlas, Morocco Jijini Rabat Oktoba 9 kabla ya kuwakaribisha Mauritania siku nne baadaye Jijini Thies.
Mechi hizo zote mbili zitakuwa sehemu ya maandalizi ya mechi za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Cameroon 2021 dhidi ya Djurtus ya Guinea-Bissau.
Kwa mujibu wa FSF, mechi zote zitachezwa bila mashabiki kuingia uwanjani kutokana na hofu ya ugonjwa wa COVID-19.
Senegal inaongoza katika Kundi I ikiwa na poniti sita baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Kongo na 4-1 dhidi ya Eswatini.
0 comments:
Post a Comment