• HABARI MPYA

    Thursday, August 13, 2020

    NEYMAR AIPELEKA PSG NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA

    Washambuliaji Kylian Mbappe (kulia) na Neymar wakishangilia baada ya kuiwezesha Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia kutoka nyuma na kuichapa Atalanta ya Italia 2-1 usiku wa jana Uwanja wa Luz mjini Lisbon, Ureno.
    Mario Pasalic alianza kuifungia Atalanta dakika ya 26 bao ambalo lilielekea kuwa la ushindi, kabla ya Marquinhos kuisawazishia PSG dakika ya 90 akimalizia pasi ya Neymar na Eric Choupo-Moting kufunga la pili dakika ya 90 na ushei akimalizia pasi ya Mbappe.
    PSG sasa itakutana na mshindi kati ya Barcelona na Bayern Munich zitakazomenyana kesho 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NEYMAR AIPELEKA PSG NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top