• HABARI MPYA

    Thursday, November 07, 2019

    JESUS AKOSA PENALTI MAN CITY PUNGUFU YATOA SARE 1-1 ITALIA

    Refa Aliaksei Kulbakov wa Belarus akimuonyesha kadi nyekundu kipa wa Manchester City, Claudio Bravo aliyeingia dakika ya 46 kuchukau nafasi ya for Ederson Moraes baada ya kumuangusha Josip Ilicic wa Atalanta dakika ya 81 wakati anakwenda kufunga timu hizo zikitoka sare ya 1-1 katika mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa wa Giuseppe Meazza mjini Milan. Kyle Walker alikwenda kusimama langoni katika mchezo ambao Raheem Sterling alianza kuifungia Manchester City dakika ya saba kabla ya  kiungo anayecheza kwa mkopo kutoka Chelsea, Mario Pasalic kuisawazishia Atalanta dakika ya 49, dakika tu baada ya Gabriel Jesus kukosa penalti 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JESUS AKOSA PENALTI MAN CITY PUNGUFU YATOA SARE 1-1 ITALIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top